Simulizi Zetu

Simulizi   Zetu

Share

17/01/2024

MOYO WA MASIKINI 💔

Sehemu ya nne🌹🌹

Simulizi zetu page

Njombe Tanzania🌹

AYUNI ANAMCHUKUA KIBA NA KWENDA NAE MJINI

Kiba alionekana mshamba sana hakuna sehemu aliyo lala macho nje ya gari muda wote ,

WANAINGIA MJINI

Kiba aliachia meno yote nje kwa mshangao " kuzuri mjini " alisema Kiba kwa sauti kubwa AYUNI alimjibu tu kwa kifupi

" kuzuri ukiwa na pesa ukipaparikia mji ni mbaya sana huu ,magorofa haya hayana msaada wowote kwako, kuna makundi ya kila aina kuna marafiki wa kila aina ,ogopa watu wa mjii huu kuliko simba na chatu mnaoishi nao kijijini , kwa sababu adui ni vizuri ukamjua kuliko akawa rafiki yako ,siku atakayo kuzuru na uaminifu wako huijui , na pia binadamu anauwezo wa kuuwa simba na chatu ,na maanisha binadamu ndio hatari kuliko simba na chatu ,na maliza kwa kusema karibu mjini KIBASU"

Kiba alikaa kimya baada ya maneno mazito ya rafiki yake , walitembea umbali kidogoo foleni ikawa kubwa Kiba akaomba msaada afunguliwe mlango mkojo umebana , kwa sababu AYUNI alitaka amtambulishe mji unasemaje akamfungulia

Kiba akawa anatafuta sehemu akojoe kila sehemu wapo watu , alizunguka sana mwisho alipata chochoro kwa bahati mbaya alishuka na begi lake na wajanja wa mjini wakajua wakuja huyu " mgeni wa mji" anamaliza kuachia kojo watu wakampora begi ikabidi aruke nao " kosa alilofanya ni kuwafuata yeye mgeni mjini"

Alikimbiza wewe wakati huo anazidi kuwa mbali na rafiki yake mwisho wale wajanja wakamzidi kete akawakosa kimoyo moyo akasema " kweli nipo mjini😂

Kiba akasema arudi alipo toka ndio akashtuka amepotea njia ya kurud amesahau , na hana simu rafiki yake nae anashanga kiba harudi akaendelea kusubiri ,akaanza kuzunguka akimuulizia kiba kwa maelezo ,jitihada zikagonga mwamba alisema tu kimoyo moyo

" wewe mtoto wa kiume pambana mpaka nitakapo kupata"

Kijijini walipata taarifa za kupotea kwa kiba waliumia sana , na hata hivyo AYUNI alitokea kumpenda sana ADA alimwekea vishawishi mwisho aliushinda moyo wa ADA

BAADA YA MIAKA 3

kiba anaonekana akiwa na mkokoteni umebeba madumu ya maji ya kutosha , anaingia nayo kwenye mgahawa na mgahawani hapo wanampokea kwa shangwe " kiba , kiba huyo , "

KIBA ALIVYO POTEA ALIPATA MSAADA KWA JAMAA MMOJA ALIYe KUWA ANAITWA RICHARD , RICHARD HUYO ALIKUWA NA MGAHAWA WAKE AMBAO NI WA KUHONGWA NA MKE WA MTU NA RICHARD PIA ANAMDOGO WAKE WA K**E ANAITWA REHEMA ,REHEMA PIA AZIPATANI NA KIBA

Kipa ananawa mikono na kuanza kutengeneza mishkaki , muda huo huo anakuja REHEMA na kuanza kufoka bila sababu ila kiba anampotezea kwa kukaa kimya

Somo kidogoo
" katika maisha jifunze kukaa kimya sababu kimya ndio jibu la kumpa mjinga , ukimjibu kwa kuongea unampa muongozo wa kukuingia, ndio maana umepewa masikio mawili mdomo mmoja , sikia sana ongea kidogo "
Tuendelee

Wakati kelele zikiendelea ghafla linakuja gari linasimama mbele ya mgahawa anashuka richi na kuagana na mwanamke mrembo ndan ya gari , yule mwanamke anamuona kiba anampungia mkono na kumsalimu " mambo kiba" kiba

Kiba anaigoma salamu kwa kukaa kimya,mwanamke anaona haitoshi anampigia simu kiba hapokea simu,mwanamke anawasha gari na kuondoka ,

Richi anafika anaingia mgahawani na anawapa hai wateja anaingia kaunta na kuangalia mauzo anakagua mazingira anamrudia kiba nje

"Vipi kiba " kiba kinyonge anajibu safi na kuiweka mishkaki vizuri ilikuwa tayari imeiva na kumuangalia usoni rafiki yake akamuuliza

" unajipenda rafiki yangu , unampenda mdogo wako , huyu mwanamke atakufikisha pabaya huyu mwanamke bwana wake anahela atakuja kukuuwa bure rafiki yangu "

Rich alikaa kimya muda Fulani na kumjibu

"Sikuelewi rafiki au unataka ukajimilikishe wewe hapa mjini ishi kwa akili , Mimi sio wewe mtu ambaye umemsubiri demu wako miaka miwili halafu unaenda kumchukua unaambiwa ameolewa yule mwanamke sio k**a ADA chali yangu nipo nae kwa miaka , sorry k**a nimekukwaza unakera ,muda wote jambo hilo tu"

KIBA alipo sikia ADA alikuwa mpole kweli ,muda huyo huyo wanasikia kelele mgahawa wa tatu REHEMA kakiwasha haswa kila dumu la maji , kiba anafika pale rehemu kashikwa roba na lijamaa huku likimkoromea , kiba alipata hasira sana

Waliwafuata na kuwaachanisha kwa nguvu akamwambia rehema tangulia akamwambia yule jamaa

" jamaa yangu usijione unamaanguvu sana Mimi sipigani kushindana , mimi napigana kutafuta heshima na weza nikakuuwa unajua nilipotea mimi , na sitaki nikuone ukimshika rehema wetu"

Rehem anaonekana akisikiliza kwa kuibia .

USIKOSE SEHEMU INAYO FUATA

12/01/2024

NILIKATA TAMAA

Sehemu ya kwanza

Ukurasa wa Simulizi zetu

"Inaanza "
Mbinguni kuna malaika wengi na malaika hao wapo katika vitengo tofauti , kuna malaika wa kusifu ambao wapo maalumu kwa ajiri ya sifa ,kuimba , kuna kitengo cha hukumu n.k ,

Kuna siku moja malaika wa sifa alikuwa akiangalia duniani na macho yake yalikuwa yakiangalia katika kijiji kimoja kinacho itwa " maana yake tupendane ,

Wanakijiji hao walikuwa wakiishi kwa amani na upendo kutokana na sababu hiyo , mungu alimtuma malaika wa kusifu hawashushie zawadi ,

, katika kijiji hiko kuna familia moja wanaonekana wakiwa katika sherehe za mavuno ambazo huwa wanakesha wakicheza ngoma na kuimba mpaka asubuhi ,

Kuna mama mjamzito alionekana akiwa katikati ya kundi la watazamaji wakifurahi ila huyo mwanamke alionekana akiwa na furaha zaidi

Muda huo huo anaonekana mume akiwa anapepesa macho anaangalia mkewe amekaa upande gani , akamuona na akamsogelea akiwa na furaha , akamuuliza

Mume " umeona kunisubiri unachelewa "

Mke " ndio yaani hapa na furaha hadi mtoto tumboni anacheza et "

Mume " kweli , acha weee ngoja nimshike , kweli amefurahi k**a mama yake "

Mke " mmh niache bhana , nataka nisoge mbele nikaone vizuri , halafu nataka mtoto wangu awe mpiga ngoma "

Mume " hata Mimi natamani "

Yalikuwa maongezi ya mume na mkewe wakiwa wanafurahia sherehe ya mavuno , basi siku hiyo ilipita

Muda wa kujifungua yule mama ulifika na mama alipata uchungu na familia yote ilikuwa karibu

Wakati mama yupo ndani na wakunga , mume alikuwa nje akisubiri mtoto kuzaliwa

Alikuja mama Mkwe na kumtia moyo mkwe wake

" nimeota mjukuu wangu ni mvulana na atakuja kufanya makubwa hapa dunia na maanisha mtoto wako atazaliwa na nyota kubwa na kipaji cha muziki niamini maneno yangu "

Yalikuwa maneno ya bibi mtarajiwa ,

Mtoto alizaliwa akiwa na afya tele ila maajabu ya mtoto baada ya kuzaliwa na kulia tu , alikaa dakika chache na kuonesha tabasamu nzuri na kunyanyua mkono wake kwa kuonesha kuitaji kugusa kitu ,

jambo ambalo lilikuwa linaendelea ulimwengu wa kiroho , malaika alishuka kumsalimu mtoto na kumpa baraka ila alikuwa haonekani kwa macho ya binadamu wengine.

KWA LEO TUNAISHIA HAPA USIKOSE SEHEMU INAYO FUATA

Endelea kufuatilia simulizi zetu hadi mwisho na usisahau kusapoti kwa comment na kushare

10/01/2024

NILIKATA TAMAA " katika maisha yetu ya kila siku tunakutana na mambo mengi sana , ya kukatisha tamaa na kutia moyo pia , simulizi yetu itamlenga kijana mmoja ambaye aliitwa KINETIAN jina ambalo alipewa na wazazi wake alipo zaliwa sababu ya kupewa jina hilo alizaliwa na baraka zote za kimila zao , kine alipewa zawadi kubwa ya kipaji cha muziki na nyota ya ajabu yenye kung'aa , alikuwa kupeteza kibaji na nyota akiwa bado anasoma shule ya msingi , na kipaji na nyota vikarudi baadae sana alipo kuwa amekataa tamaa ,akiwa kwenye wakati mgumu ,heshima ,umarufu , vikamrudi waliomkataa mwanzo wakaamuona dhahabu , ila kabla hajarudishiwa kuna masherti alipewa na malaika , na aliyakosea na mwisho wake ukawa mauti
.Masharti gani Alipewa ?.Kipaji na nyota nani alichukua ? Na vilirudije ?.Vipi kuhusu mahusiano ya kimapenzi ? " kuna lovestory Kali kinoma humu ndani "
Mnamengi ya kuyajua sio muda mrefu inakuja katika sauti na maandishi ..

Want your business to be the top-listed Engineering Company in Njombe?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Telephone

Website

Address


Njombe