Kitambo Inspiration
10/06/2026
UMEDANGANYWA NA WA SDA NAOMBA NIKUSAIDIE RAFIKI YANGU
Shalom wapendwa
Kwa Leo naomba nimsaidie rafiki yangu huyu na yeyote mwenye fikra k**a hizi..
Katika ujumbe wake alioutoa ameeleza kwamba Bwana wa sabato anakuja na ili tuwe salama tunapaswa kushika sabato ndo mhuri wake..
Akatoa maandiko ..Ezekieli 20:20, kum31:15-18, isaya58:13-14 nk
SASA TWENDE SAWA
1.kosa kubwa ambalo linawatesa wasabato na litaendelea kuwatesa ni kushindwa kutafsiri mkutadha ..yaani ujumbe mkuu , lini? Kwetu tufanye nini nk
Kwahiyo wao wanachukua kamstari kamoja tu na kutembea nako ...Imesalia raha ya sabato... Au sabato imefanyika kwa wanadamu...
2.katika maandiko hayo aliyotaja hakuna hata moja la agano la jipya..ndio maana nilisema hawa wasabato wanajifanya kumtukuza Kristo lakini ihalisia wamefungamana na mafundisho ya misa
3.Agano jipya limeweka wazi kwamba mhuri wetu ni Roho mtakatifu...
Sasa hawa jamaa unaweza kujiuliza kwanini hawataki kumnadi Roho mtakatifu?? Ilihali Yesu anaondoka atakuja msaidizi ROho mtakatifu ...yohana14:26
Na pia paulo natuweka bayana kwamba mhuri wetu tunaupata kwa Roho mtakatifu..si kwa kusali siku ya jumamosi..AMKENI
Waefeso 4:30
[30]Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi.
4.Jambo la kujiuliza dogo sana ..kwamba k**a sabato ingekuwa lazima au mhimu kiasi hicho k**a wanavyotuelezea ndugu zetu wasabayo ...
Kwanini Yesu hakuna mahali aliagiza au kusiaktiza wafuasi wake kuishika sabato??
Baada ya ukristo kuanza nyaraka nyingi zilizoandikwa na mitume ...za Paulo, yo ha na, petro ,yuda nk kwanini hakuna hata mmoja aliyewakumbusha au kuwasisitiza kuishika ??
K**a ingekuwa mhimu au lazima kwa wakristo naamini wangesisitiza ...
Mbona sheria zingine au amri zingine k**a :usiibe , usiabudu sanamu, usizini nk zimeagizwa kwa wakristo na Yesu au nyaraka za mitume lakini hakuna agizo la kuendelea kushika sabato?? Je Walijisahau ? Walipuuza??
AMKENI AMKENI AMKENI
Mungu awabariki
04/06/2026
KIGOMA MWAKEYE TUMEWAFIKIA
04/06/2026
Usihukumu watu kwa makosa yao ya jana ,watu hubadilika ,watu huinuka tena upya na kufanya vizuri
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the public figure
Telephone
Address
Isamilo
Mwanza