Wami Ruvu Basin

Wami Ruvu Basin

Share

Photos from Wami Ruvu Basin's post 19/02/2024

Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu inatekeleza mradi wa kutengeneza Mfumo wa kutabiri Mwenendo wa Maji katika Mto Ruvu utakaosaidia kufanya utabiri wa majanga ya mafuriko na ukame na kisha kutoa taarifa kamili zitakazotumiwa na wadau mbalimbali wanaotegemea maji ya mto huo katika shughuli zao za kichumi na kijamii.

Akizungumza katika warsha fupi ya kufunga mafunzo yaliyodumu kwa siku 7 yaliyotolewa na mtaalamu mshauri kutoka M/S DIT ya kuwajengea uwezo watalaam kutoka Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu juu ya uendeshaji wa mfumo huo, Mkurugenzi wa Rasilimali za Maji Dkt. George Lugomela ameipongeza Wami/Ruvu kwa kuja na Mradi huu utakaoweza kutoa taarifa za awali juu ya majanga mbalimbali yanayosababishwa na mabadiliko ya Tabia Nchi.

Dkt. Lugomela ameitaka Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu kutekeleza kwa weledi mradi huu na kuwa chachu ya kutoa mafunzo kwa Mabonde mengine hapa nchini

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu Mhandisi Elibariki Mmassy amebainisha kuwa Mfumo huo utaweza kutabiri kila baada ya siku 10 lengo likiwa ni kupata taarifa sahihi kutokana na umuhimu wa Mto Ruvu.

Mradi huu wa mfumo wa kutabiri mienendo wa maji mtoni unatekelezwa kwa fedha kutoka Benki ya Dunia kwa kupitia Mradi wa Kusaidia Sekta ya Maji (WSSP II) unaogharimu kiasi cha Shilingi Milioni 325,700,000.

12/01/2024

Heri ya siku ya Mapinduzi…!!

Want your organization to be the top-listed Government Service in Morogoro?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Website

Address


Mazimbu Road
Morogoro