BWAY MEDIA
27/03/2026
Whom am I?
28/04/2023
Mashambulizi ya anga ya Urusi yameshambulia miji kote Ukraine, ukiwemo mji mkuu wa Kyiv, na kuua takriban watu watano. Mwanamke na mtoto wa miaka mitatu waliuawa katika jiji la Dnipro, kulingana na meya wa eneo hilo. Watu watatu walikufa huko Uman baada ya makombora kugonga majengo ya makazi, maafisa walisema. Jengo la ghorofa tisa hapo liliharibiwa vibaya. Kulikuwa pia na milipuko katika miji ya Kremenchuk na Poltava, kulingana na shirika la habari la Interfax. Mjini Kyiv, makombora 21 kati ya 23 na ndege zisizo na rubani mbili zilidunguliwa na mfumo wa ulinzi wa anga wa Ukraine, maafisa walisema katika chapisho la Telegram.
Mkuu wa utawala wa kijeshi wa mji wa Kyiv alisema hilo lilikuwa shambulio la kwanza la kombora la Urusi katika mji mkuu katika muda wa siku 51. Hakuna ripoti za mara moja za vifo vya raia katika mji mkuu. Mashambulizi hayo yametokea huku vikosi vya Ukraine vikiaminika kujiandaa kwa mashambulizi ya kijeshi na vifaa vipya, vikiwemo vifaru, vilivyotolewa na washirika wa nchi za Magharibi.
Urusi imejitahidi kupiga hatua katika mashambulizi ya majira ya baridi ikiwa ni pamoja na vita vya miezi 10 vya kuudhibiti mji muhimu wa kimkakati wa mashariki wa Bakhmut
https://instagram.com/bway2032?igshid=ZDdkNTZiNTM=
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Address
Gairo
Morogoro