Bawasiri Therapy

Bawasiri Therapy

Share

08/01/2025

Bush Diet...

08/01/2025

Leo nataka nizungumzie Suala Moja ambalo

Linawatesa Wengi Sana Kila Siku

Hasa Hasa kwa Watu Wenye Changamoto ya Bawasiri

✅ Kupata Choo Kigumu Sana.
Hali ambayo Inamfanya Mtu atumie Nguvu nyingi Sana

Wakati wa Kujisaidia Haja Kubwa

✅ Kupata Maumivu Makali Sana Wakati wa Kujisaidia Haja Kubwa

Kwa Sababu ya Kile Kinyesi Kinakwangua Vile Vinyama

Katika Njia ya Haja Kubwa na hii Hali Inaweza Kupelekea

Kuota Vinyama Vingine Tena

unakuta Mtu ana Vinyama Zaidi ya Viwili au Vitatu

Katika Tundu la Haja Kubwa

Kwa Sababu ya;

''Choo Kigumu ''

✅ Kutumia Nguvu nyingi Sana.
Kikawaida Mtu anavyojisaidia Inabidi atumie

Misuli ya Tumbo Ku- Push Haja Kubwa

Lakini K**a Choo ni Kigumu Sana

Itamlazimu atumie Misuli ya Mwili Mzima

Kwa Nguvu Zote...

Unakuta Mpaka Mishipa ya Kichwani Kwenye Komwe

Imevimba Ili Mtu apate Choo

Mpaka Mtu amalize Tayari Kachoka Vibaya Mno

Mpaka
" Kizungu zungu "

Hayo ni Baadhi Tu ya Madhara ya Kutumia sukari

Yaani

Vinywaji Vyenye Sukari Sana

Mfano;
🚫 Soda Nyeusi
🚫 Juisi zaViwandani
🚫 Energy Drinks

Pia na Vyakula Vyenye Sukari Sana

Mfano;
🚫 Keki
🚫 Maandazi
🚫 Mikate ya Viwandani

Kwa Ushauri Zaidi

Kwa Wale

Wenye Matatizo ya Kupata Choo Kigumu

au

Kutopata Choo Kabisa

Wasiliana nami

'' *0766 931 400* ''

Mtindo wako wa Maisha,

Ni Wewe,

Unae amua.

"Epuka Sukari"

Mshauri Wako,

Mwankenja Adam...

05/09/2024

Watu Wengi Huwa Tunakosea Hapa
Kwenye Suala la Matunda
Na ni Kitu Ambacho Kimezoeleka Sana
Kula Matunda Baada ya
Kula Chakula
Sasa Leo Nikupe Somo Kidogo
Ndani ya Sekunde 60 Zijazo
Utaenda Kujifunza Siri Muhimu
Ya Ulaji Mzuri wa Matunda
Twende Kazi...

Matunda inabidi Yaliwe Kabla ya Kula Chakula
Tena Yaliwe Saa Moja Kabla ya Kula Chakula
Najua Unajiuliza Kwanini?
Ok Vizuri Sana
Matunda ni Rahisi Sana
Kumeng'enywa au Kusagwa
Na Virutubisho Vyake Kufyonzwa Ndani ya Mwili
Ikiwa Tumbo Litakuwa Empty
Yaani Tumbo Halina Chakula
Ukifanya Hivi Utakuwa
Umefanya Mwili Kuweza Kupata
Vitamins na Madini Yatokayo
Kwa Matunda Kiurahisi Zaidi
Lakini Watu Wengi Huwa Wanakula Matunda
Baada ya Kula Chakula Kitu Ambacho
Sio Sahihi Kwa Mwili
Kwanini?
Kwa Sababu...
Ukila Chakula afu Ukala Matunda
Haya Matunda Yanakuw ni Vigumu
Kumeng'enywa au Kusagwa
Kwa Sababu Yamekutana na
Chakula Kizito Tayari Tumboni
Hivyo Basi Vitamins na Madini Yaliyopo
Kwenye Hayo Matunda Hayatafyonzwa Mwilini
Kwa Hiyo Utakuwa Umeupa Tu Mwili
Mzigo Mzito Sana wa Kufanya Umeng'enyaji wa Chakula
Pamoja na Matunda
Ngoja Nikuulize Swali Kidogo?
Hivi Ushawahi Kula Chakula afu Baada ya Hapo
Ukala Tikiti Maji?🍉
Ulijisikiaje??
Najua Hii Experience Kila Mtu Anayo
Yah Ulihisi Tumbo Limejaa Sana...
Ila Ungeanza Kula Tikiti Maji afu Baadae
Ukala Chakula Inakuwa ni Vizuri Zaidi
Na Hii Itakufanya Usile Chakula Kingi Sana
Na Hii ni Nzuri Sana Kwa Wale Ambao Hawataki
Kuongezeka Uzito wa Mwili
Kwa Leo Tuishie Hapo
Kula Matunda kwa Afya Yako
Mshauri Wako
Adam Mwankenja...

04/09/2024

Changamoto Nyingine Kubwa Zaidi
Ambayo Inawasumbua Watu Wengi
Wenye Tatizo la Bawasiri
Ni, Kuharisha
Suala la Kuharisha ni Suala la Kawaida
Ambalo Linamtokea Kila Mtu na Muda Wowote
Bila Kutarajia
Lakini Hili Suala Tunaweza Tukalipunguza
Ka Kiasi Fulani Ili Tusipate Majanga Zaidi
Hasa Hasa Kwa Mtu Mwenye Bawasiri
Huwa Inakua ni Hatari Zaidi
Kwa nini? Utauliza
Ok Vizuri Kwa Kuuliza
Kwa Sababu
Kitendo cha Kuharisha Huwa Kinasababisha
Maumivu Makali Sana Kwa Bawasiri
Au Vile Vinyama Katika Njia ya Haja Kubwa
Yaani Haya Maumivu Huwa Yanakuwa Mara Saba Zaidi
Ya Maumivu Kawaida
Inaweza Kupelekea Mtu Asiweze ata Kuketi
Kwenye Kiti Kwa Sababu ya Maumivu Makali
Hivyo Basi
Hakikisha Unakula Chakula Salama Kwa Tumbo Lako
Hata K**a Unakula Mgahawani
Hakikisha Unachagua Mgahawa Mzuri na Msafi
Ni Bora Ugharamie Chakula Ghali ata Kwa 15,000/=
Kuliko Kula Chakula cha 3000/=
Ukaharisha na Kuishiwa Maji Mwilini
Na Kwenda Kulazwa Hospitali na Kulipa Gharama Zingine
Zaidi ya Ile ya Kugharamia Chakula
Kwa Hiyo Hakikisha Una Kuwa Selective
Yaani Uwe Mtu Mwenye Uwezo wa Kuchagua
Nile nini? Nisile Nini?
Nile Wapi? Nisile Wapi?
Kula Salama Kula Vizuri
Mshauri Wako
Mwankenja Adam

Want your practice to be the top-listed Clinic in Mbeya?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address


Mbeya
53220