Mbeya Polytechnic College
14/02/2017
TANGAZO LA MASOMO YA BIASHARA NA UHASIBU
MBEYA POLYTECHNIC COLLEGE-VOCATIONAL
TRAINING CENTRE (MPC-VTC)
Mkuu wa Chuo cha Mbeya Polytechnic, kwa niaba ya Bodi ya Ushauri; anawatangazia WANAFUNZI waliomaliza Kidato cha Nne nafasi ya kujiunga na masomo ya NABE katika Ngazi ya NABE STAGE I, STAGE II na STAGE III; kwa muhula mpya wa masomo utakaoanza tarehe 1 Machi, 2017.
Chuo cha Mbeya Polytechnic kimepewa Usajili na VETA kuendesha kozi hii kwa barua yenye Kumb. Na. VETA/SWRS/VTC/PTC/MBY/2.35/11 ya tarehe 8 Februari, 2017, kutoa mafunzo katika fani za Biashara na Uhasibu (NABE) yatakayofundishwa kwa kipindi cha Miezi Sita (6) kila ngazi. Wahitimu wa STAGE III, watajiunga na vyuo vya Biashara vilivyo chini ya NACTE, kuendelea na Ngazi ya Cheti, Diploma na Digrii.
Sifa za kujiunga ni: Mwanafunzi yeyote aliyemaliza Kidato cha Nne na kuendelea.
Chuo kipo katika jiji la Mbeya, Kata ya Iganzo.
Kwa mawasiliano na msaada zaidi tembelea tovuti yetu www.mbeyacollege.ac.tz au simu namba 0754-324 030 / 0764-774 929 / 0783-362 553 au 0714-147 353.
MBEYA POLYTECHNIC COLLEGE-VTC
“ TO LEARN IS TO CHANGE.”
Mbeya Polytechnic College Having the right skills is very important in today’s competitive job market. With Mbeya Polytechnic College, you’re assured of learning career skills that will prepare you for the jobs of today and tomorrow.
22/01/2017
Moja ya Somo linalofundishwa Chuoni kwetu kwenye kozi ya Kilimo na Mali asili kwenye Kampasi ya Tukuyu ni
UFUGAJI WA SAMAKI (Aquaculture au aquafarming),
UFUGAJI WA SAMAKI ni kilimo cha viumbe vinavyoishi majini, kwa mfano samaki, konokono na mimea ya majini. Aquaculture inahusisha kilimo cha viumbe vinavyoishi kwenye maji baridi na vile vinavyoishi kwenye maji ya chumvi katika mazingira ya kuhudumiwa,
Katika kozi ya Aquaculture Chuo kinafundisha elimu ya ufugaji wa samaki, ikiwa ni pamoja na utengenezaji wa mabwawa, utotoleshaji wa vifaranga vya samaki, namna salama ya kusafirisha vifaranga vya samaki, namna ya kuwapanda na kuwahifadhi samaki katika mabwawa na pia usimamizi wa mabwawa (ikiwa ni pamoja na kujifunza magonjwa mbalimbali ya samaki na tiba zake).
USIMAMIZI WA UVUVI (Fisheries management):
Usimamizi huu hujikita zaidi katika sayansi ya uvuvi wa samaki ili kutambua njia sahihi za kulinda maliasili samaki na uvunaji wake uwe wenye mafanikio na endelevu.
Sayansi ya Uvuvi wa Samaki ni taaluma inayohusu uelewa na usimamizi wa uvuvi. Ni sayansi yenye upana katika nyanja za elimu ya maji baridi (mito, mabwawa, visima, n.k.; na maji chumvi ya bahari (limnology, oceanography, freshwater biology, marine biology, conservation, ecology, population dynamics, economics na management),
Chuo kinamtayarisha mwanachuo katika usimamizi na utunzaji wa maliasili samaki kwa kufanya shughuli za uvuvi katika mito, maziwa na bahaari. Halikadhalika Chuo kinamfundisha mwanachuo matumizi ya vifaa vya uvuvi, utengenezaji wa vyombo vya kuvulia, :.nyavu za kuvulia n.k. Pia Chuo kinamfundisha mwanachuo mbinu bora za uvuvi na usimamizi wa uhifadhi wa maliasili samaki kulingana na sheria na kanuni za kitaifa na kimataifa.
01/06/2016
Convince yourself you want to do it. ...
Take control. ...
Surround yourself with other people who are working hard. ...
Break up your tasks into smaller tasks. ...
Stay focused. ...
Remember your "why." ...
Stay positive.
14/05/2016
Karibu ujisajili kwenye Chuo chetu kupitia hawa Business partners wetu bila gharama za ziada!
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the school
Website
Address
IGANZO
Mbeya
Opening Hours
| Monday | 08:00 - 21:30 |
| Tuesday | 08:00 - 21:30 |
| Wednesday | 08:00 - 21:30 |
| Thursday | 08:00 - 21:30 |
| Friday | 08:00 - 21:30 |