Daniel awack

Daniel awack

Share

17/05/2026
07/04/2026

KARATU IMEPOTEZA WATU MAKINI SANA

Photos from Daniel awack's post 10/03/2026

Nimeshiriki kikao cha 52 cha Bodi ya Barabara ya Mkoa kilichofanyika tarehe 9 Machi 2026, ambapo pamoja na agenda nyingine muhimu, kikao hicho kimeridhia kupandisha hadhi ya barabara ya Rhotia – Kambi ya Simba – Slahhamo – Kitete – Upper Kitete – Lositete hadi Selela, Monduli. Barabara hiyo ambayo hapo awali ilikuwa inahudumiwa na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), sasa inapendekezwa kuhamishiwa kuhudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) ili kuboresha zaidi miundombinu yake na kuongeza ufanisi wa huduma kwa wananchi.
Hoja ya kupandisha hadhi ya barabara hiyo iliwasilishwa mapema tarehe 6 Machi 2026 mbele ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mwigulu Lameck NCHEMBA, wakati wa ziara yake Wilayani Karatu, mkoani Arusha. Kupitishwa kwa pendekezo hilo kunatarajiwa kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa maeneo ya Rhotia, Kambi ya Simba, Slahhamo, Kitete, Upper Kitete, Lositete na Selela, kwa kurahisisha usafiri na usafirishaji wa bidhaa pamoja na huduma muhimu.
Hatua hiyo inaenda sambamba na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan za kuendelea kuboresha miundombinu ya barabara nchini kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

Want your public figure to be the top-listed Public Figure in Karatu?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address


Karatu