Habari Za Soka
27/11/2025
DIEGO MARADONA, MCHEZAJI BORA KUWAHI KUTOKEA KWENYE MIOYO YA WATU
Mkondo wa maji machafu, kelele za risasi, nyumba za kubanana, watu wengi mpaka hakuna pa kutema mate, udokozi, madawa na vijana wenye silaha mifukoni kila siku Mapolisi wapo doria, ni mitaa iliyomlea Maradona pale Villa Fiorito Jijini Buenos Aires, Argentina
Maradona anakua bila kupata muda mrefu wa kukaa na Baba yake Don Diego, anaamka saa 10 Alfajri na kurudi saa sita usiku, akirejea nyumbani alikuwa ni k**a mfu alie hai, mafukara walivyogundua kipaji chake walimpeleka Boca Juniors, ndio inaaminika ni klabu ya asili yao
Wakati Maradona anaelekea Ulaya, alifikia FC Barcelona ambapo hapo alicheza kwa miaka miwili chini ya Rais mbabe Nunez, hakupata upendo mkubwa sana na walipenda kumbagua na kumwita 'Sudaca' wakimaanisha mtu mweusi wa America Kusini
Aliwahi kuwaambia Wawakilishi wake kuwa hajisikii raha kucheza Barca mbele ya matajiri, wamtafutie timu yoyote yenye watu fukara, waliochoka maisha na hawana uhakika wa kula, anataka kuwa Nuru kwenye giza la maisha yao, alimaliza k**a haipo hiyo timu Ulaya basi arudi Boca Juniors
Ilikuwepo timu moja kutoka Kaskazini mwa Italia, ambapo watu wake maisha magumu, serikali inauchukia mji wa Naples watu waliishi bila uhakika wa kesho yao, ndipo ndani ya Mji huo kulikua na klabu ya SSC Napoli, ndipo hapa kuna ladha k**a za mitaa ya kwao Argentina
Ilimlazimu Mkurugenzi wa Napoli Antonio Juliano ambae pia alikulia maisha ya dhiki na shida Naples, kusafiri mpaka Barcelona kukamilisha dili la Maradona, kitu pekee alimwambia Diego ni kuwa hapa utakua kati ya miungu wanaoishi, tutakupa heshma zote,
Wakati Juliano anakubaliana dau la rekodi ya uhamisho duniani, Rais wa Barca alidai nyongeza ya pauni laki tano, ilibidi Juliano arudi Naples kuwatangazia Wananchi kuwa kiasi hicho kinahitajika na klabu haina pesa, Mashabiki na raia wa Naples wakaanza kuchangishana
Watoto, vijana na wazee chochote kilichopo mfukoni wanatoa ili Diego aje Naples, kuanzia Camorra mpaka mitaa ya Forcella, kila mtu licha umaskini na wengine inasemekana walikosa hata chakula ili kutoa kwa ajili ya usajili.
26/11/2025
✍Ilikua ukikutana na timu iliojaa wahuni ya Stoke City tena kwenye lile dimba lao la Britannia Stadium naongelea kipindi kile Stoke city kweli ya wanaume tena majira Yale ya baridi barani ulaya
✍Ilikua wakipata mpira wa kurusha kuna muhuni mmoja wa kuitwa Rory Delap huyu alikua bingwa wa kurusha mipira aliandaliwa hadi taulo kwajili ya kufuta mpira kabla ya kurusha
✍Moja ya mchezaji aliekua akichukiwa sana na Arsenal Wenger ni huyu kutokana hio style yake mpira unarushwa utafikiri kapiga kwa mguu
✍Crouch,Jonathan Walter,Ricardo Fuller & Kenwayne Jones walifaidika kwa kiasi kikubwa sana na mipira hiyo wakati huo stoke chini ya mwalimu Tony Pulis
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the public figure
Website
Address
Sabasaba
Iringa