Taifa Digital Forum

Taifa Digital Forum

Share

19/05/2025

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameitaka Wizara ya Mambo ya Nje, Wizara ya Mambo ya Ndani na Vyombo vya Ulinzi na Usalama kuchukua hatua za haraka kwa wanaotumia mitandao na teknolojia vibaya, akikemea pia wingi wa Wanaharakati kutoka nje ya nchi wanaojaribu kuingilia mambo ya ndani ya Tanzania na kutaka kuivuruga amani.

Rais Samia amesema hayo Jijini Dar es salam leo May 19, 2025 wakati akizindua Sera ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001 (Toleo la 2024), ambapo amesema hatotoa nafasi kwa watovu wa adabu kutoka nje ya nchi kuja kujaribu kuvuruga amani, utulivu na usalama uliopo nchini Tanzania.

“Tusiwe shamba la Bibi kwamba Mtu anaweza kuja Tanzania akasema analolitaka, lipo Tanzania halipo, Watu wakajisemea tu, tumeanza kuona mwenendo wa Wanaharakati ndani ya Ukanda huu kuanza kuvamia na kuingilia mambo yetu huku, sasa k**a kwao wameshadhibitiwa wasije kutuharibia, tusitoe nafasi walishavuruga kwao, nchi iliyobaki haijaharibika ni hapa kwetu, niwaombe Vyombo vya Ulinzi na Usalama kutotoa nafasi kwa Watovu wa adabu wa nchi nyingine kuja kutovuka hapa kwetu, hapana”

“Nimeona clip kadhaa za kunisema, nipo bias na nini, ninalofanya ni kulinda nchi yangu na ndiyo wajibu wangu niliopewa, kwahiyo hatutotoa nafasi kwa kiumbe yeyote kuja kutuvurugia hapa awe yupo ndani ama anayetoka nje”

Katika maelezo yake, Rais Samia ameitaka Wizara na Maafisa wanaohusika kutoa ufafanuzi kuhusu yale yanayosemwa na Wanaharakati na Watu mbalimbali, kukanusha ama kuchukua hatua za haraka ikiwa yanayosemwa yana ukweli kuhusiana na sekta zao mbalimbali.

19/05/2025

RAIS SAMIA AWAKARIBISHA DIASPORA NA RAIA WA KIGENI KUWEKEZA NCHINI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amewakaribisha Watanzania wanaoishi Nje ya nchi maarufu k**a Diaspora pamoja na Raia wa Kigeni na Sekta zao binafsi kuja kuwekeza nchini Tanzania, akieleza kuwa sasa Sera ya Mambo ya nje inawatambua rasmi k**a wabia muhimu wa maendeleo ya Tanzania.

Aidha Rais Dkt. Samia ameeleza kuwa uhusiano na Diplomasia ya Kimataifa ni suala linalohusu pia ulinzi na usalama wa nchi hivyo ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama nchini Tanzania kuhakikisha kuwa wanajidhatiti katika kudhibiti vitendo vya uhalifu wa kuvuka mipaka pamoja na matendo ya kigaidi yanayoendelea kote duniani kwa kuhakikisha mipaka inakuwa salama na amani inatamalaki nchini.

Rais Samia amebainisha hayo leo Jumatatu Mei 19, 2025 kwenye Hafla ya uzinduzi wa sera ya mambo ya nje ya Mwaka 2001, toleo la mwaka 2024, akiwahamasisha Watanzania wanaoishi nje ya nchi kuwa mabalozi wema wa Tanzania kwa kutangaza mazuri na fursa zinazopatikana nchini Tanzania.

Aidha Rais Samia ametoa wito kwa watanzania hususani Vijana pamoja na sekta binafsi nchini, kuchangamkia fursa mbalimbali za kiuchumi na kijamii zilizopo nchini, akizitaka Mamlaka zinazosimamia ajira nje ya nchi kuja na sera na sheria rafiki kwa Watanzania ili waweze kufaidika na mahusiano mema ya Tanzania na Mataifa mengine ambayo yamekuwa yakitoa fursa za ajira kwa raia wa kigeni.

19/05/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Sera ya Mambo ya Nje ya mwaka 2001 Toleo la Mwaka 2024 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 19 Mei, 2025.

19/01/2025

Mtaalam na mchambuzi wa masuala ya Siasa na mai Maendeleo Dkt. Dennis Muchunguzi amemwagia sifa Makamu Mwenyekiti wa CCM bara Ndugu, Stephen Wasira baada ya kuchaguliwa kwa Kishindo na wajumbe wa Mkutano mkuu Maalum wa CCM uliofanyika jana Tarehe 18 Januari 2025 katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

06/07/2024

Mchambuzi wa masuala ya kisiasa na kiuchumi nchini Dkt Denis Mchunguzi ameeleza kwa undani zaidi tukio la aliyekuwa mbunge wa Iringa mjini na kada maarufu wa CHADEMA Mchungaji Peter Msigwa kuamia CCM.

Want your business to be the top-listed Media Company in Dodoma?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Website

Address


Dodoma