Institute of Rural Development Planning (IRDP)
25/03/2026
TANZIA
18/03/2026
ZANA ZA KISASA ZIKAWE CHACHU YA ONGEZEKO LA THAMANI YA ZAO LA MWANI NCHINI-Mhe. Nderiananga
Na; Sweetbetter Njige-Tanga
Vikundi vya Wakulima wa zao la Mwani Wilayani Mkinga vyahimizwa kutumia fursa ya uwepo wa zana za kisasa za kuchakata zao la mwani kuongeza thamani ya zao hilo
Rai hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Mheshimiwa Ummy H. Nderiananga (Mb) Machi 16, 2026 katika hafla ya makabidhiano ya mashine mbili zenye uwezo wa kusaga kilo 500 kwa saa na kaushio moja lenye uwezo wa kukausha tani nne kwa mara moja kwa vikundi vya wakulima katika Kijiji cha Kichaka Mimba, wilayani Mkinga mkoani Tanga.
“Lengo la Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuendelea kushirikiana na wadau mbali mbali wa maendeleo ili kuhakikisha uchumi wa blue una kuwa kupitia mazao ya bahari na unaimarisha mnyororo wa thamani kuanzia kwenye kuzalisha hadi kuchakata mazao haya hivyo basi, nitoe rai kwenu wakulima kuhakikisha mnatumia zana za makaushio na mashine kwa ufanisi ukubwa ilimuweze kukuza uchumi wa kaya moja moja na vikundi vya wakulima kwa ujumla” Alisema Mhe. Nderiananga (Mb)
Aidha, Mheshimiwa Nderiananga amewashukuru UNDP na Serikali ya Japani kwa kushirikiana na Serikali kutengeneza mazingira wezeshi kwa vikundi vya wakulima wa mwani.
Akitoa utangulizi wa mradi, Mkurugenzi wa Kituo cha Mafunzo cha Kanda ya Ziwa Prof. Juvenal Nkonoki amesema tathmini ilibaini changamoto za mbinu duni za kilimo, ukosefu wa miundombinu na elimu kwa vikundi, na kuanza kutatuliwa kupitia mafunzo yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini kwa ufadhili wa Serikali ya Japani na UNDP.
Naye mkuu wa Wilaya ya Mkinga Mhe. Gilbert Kalima amewashukuru wafadhili na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kuratibu upatikanaji wa zana za kuchakata mwani zitakazoongeza thamani ya zao hilo na kuwainua kiuchumi wakulima huku akiahidi kuendelea kutoa ushirikiano na mazingira rafiki kwa wakula na wadau ili kufikia malengo.
17/03/2026
Mratibu wa Mradi wa Mageuzi ya Kiuchumi kupitia Elimu ya Juu (Higher Education for Economic Transformation-HEET), Bw. Said Abdallah Panga (kulia), akifuatilia Mafunzo ya Maandalizi ya Makabidhiano na Kufunga Mradi, ambapo leo ni siku ya pili ya mafunzo hayo.
Mafunzo haya yanaendeshwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (MoEST) na yanafanyika katika Ukumbi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) uliopo Morogoro.
Lengo la mafunzo haya ni kuwaandaa wadau wa mradi katika hatua za mwisho za utekelezaji, ikiwemo taratibu za makabidhiano, tathmini ya mafanikio, na kufunga rasmi mradi wa HEET.
08/03/2026
HERI YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI.
“Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana: Msingi Jumuishi kufikia Dira 2050”
💪💪💪
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the university
Telephone
Website
Address
Miyuji
Dodoma
138DODOMA,
Opening Hours
| Monday | 08:00 - 15:30 |
| Tuesday | 08:00 - 15:30 |
| Wednesday | 08:00 - 15:30 |
| Thursday | 08:00 - 15:30 |
| Friday | 08:00 - 15:30 |