WCWSA
26/02/2026
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto mhe Anna Athanas Paul amewataka wanafunzi wa Skuli ya Jendele kuendelea kujilinda na kujitunza ili waweze kujikinga na vitendo vya ukatili na Udhalilishaji wa kijinsia.
Mhe Anna ameliyasema hayo wakati akigawa taulo za k**e za kufua kutoka katika kampun ya safe Pad kwa wanafunzi wa Skuli ya Jendele wilaya ya kati mkoa wa kusini Ungujà.
Mhe Anna pia amewataka wanafunzi hao kusoma kwa bidii ili waweze kuwa viongozi bora kwa taifa la baadae.
20/02/2026
Jana mapema taasisi yetu ya ikishirikiana na wadau wetu wazalishaji wa taulo za k**e/pedi za kufua za SafePad walitembelea skuli ya Jendele Secondary wakiambatana na Mheshimiwa Waziri wa Wizara Mh. Anna Athanas Paul.
Mheshimiwa Waziri na wageni wetu wakiambatana na timu ya WCWSA waliweza kupata fursa ya kutumia muda wao na wanafunzi 100 wa skuli ya Jendele.
Wanafunzi wa k**e 100 hao waliweza pia kupatiwa taulo za k**e za kufua na baadhi ya vitendea kazi vya kuwasaidia wanapokuwa shuleni.
Shukrani za dhati kwa wageni wetu hususani bi na familia yake kwa kuwezesha misaada hiyo kufikia shule ya Jendele na shukrani kwa serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kuunga mkono jitihada hizi za kumsaidia mtoto wa k**e abaki shuleni.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the organization
Telephone
Website
Address
Dodoma