Taifa Choice

Taifa Choice

Share

Photos from Taifa Choice's post 08/08/2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimvisha taji Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb) wakati wa hafla ya makabidhiano ya zana za kilimo kwa Wizara ya Kilimo ili kuendelea kuhamasisha matumizi bora ya zana za kisasa ili kuongeza tija na uzalishaji nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Bashe amesema Wizara ya Kilimo imeanza kujenga Vituo Jumuishi vya Zana za Kilimo (mechanization Centers) ili kumsaidia mkulima kuweza kupata huduma hiyo kwa urahisi.

Jumla ya trekta 119 za aina ya Swarage zenye horsepower tofauti tofauti zimekabidhiwa, power tiller 800 pamoja na majembe 200 kwa ajili ya maandalizi ya mashamba.

Photos from Taifa Choice's post 03/08/2024

SILINDE AHAMASISHA MATUMIZI YA ZANA BORA ZA KISASA KWENYE KILIMO

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb) amesema Wizara imedhamiria kuwawezesha Vijana katika Sekta ya Kilimo kwa kuwapatia zana mablimbali ikiwemo matrekta waweze kulima kwa tija.

Mhe. Silinde amesema hayo wakati akikabidhi matrekta 09 kwa wakulima kutoka Kampuni ya PASS Leasing Company Limited katika Maonesho ya Kilimo ya Kimataifa yanayofanyika katika Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma leo tarehe 03, Agosti 2024.

"K**a serikali tumejipanga katika kuhakikisha vijana wanapata uelewa kuhusu kilimo na tayari tushatoa maelekezo kwa Mikoa na Halmashauri zote nchini kutenga maeneo kwajili ya vijana ili Taifa letu la Tanzania lijitosheleze na mazao ya kilimo". amesema Silinde

kwa upande wake Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya PASS Leasing Limited, Rosebud Kurwijila amesema kampuni hiyo imekabidhi vifaa vya kulimia kwa wakulima zikiwemo trekta 9 zenye thamani millioni 401.76 kwa wakulima wa mkoa wa Dodoma, wilaya ya Kongwa na Chemba.

"Uwezeshaji huu tunategemea utakwenda kuongeza uzalishaji kwa kulima mashamba zaidi ya ekari 2000; kutengeneza ajira za moja kwa moja zisizopungua 30 na kuwafikia wanufaika takribani 300 kwa kipindi cha msimu mmoja". amesema Rosebud Kurwijila

Wizara ya Kilimo imeendelea kuhamasisha matumizi ya zana bora za killmo ikiwa ni pamoja kujenga uwezo wa zana za kilimo na kuwawezesha wakulima kuwa na uhakika wa zana wanazotumia katika shughuli zao za kilimo ili kufkkia dhamira ya Serikali kufikia matrekta 10,000 ifikapo mwaka 2030.

Photos from Taifa Choice's post 01/08/2024

BASHE: MATREKTA 500, POWER TILLER 800 KUZINDULIWA KATIKA MAONESHO YA NANE NANE 2024

Zaidi ya matrekta 500 na power tiller 800 zitazinduliwa wakati wa Maonesho ya Kilimo ya Kimataifa ya Nane Nane 2024 ikiwa ni sehemu ya matrekta 10,000 yanayotarajiwa kununuliwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb) amesema hayo wakati wa Hafla ya Ufunguzi wa Maonesho hayo tarehe 1 Agosti ya Nane Nane 2024 yanayofanyika Kitaifa Mkoani Dodoma, katika viwanja vya Nzuguni.

Hatua hiyo ni kujenga uwezo wa zana za kilimo na kuwawezesha wakulima kuwa na uhakika wa zana wanazotumia katika shughuli zao za kilimo.

Waziri Bashe amesema kuwa dhamira ya Serikali ni kufikia matrekta 10,000 ifikapo mwaka 2030.

Want your business to be the top-listed Media Company in Dodoma?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Address


Dodoma