Tmcs-cbe

Tmcs-cbe

Share

26/04/2022

Neema isiyo na kikomo imetolewa ili roho iaminiyo iweze kuwekwa huru na dhambi; kwa maana mbingu zote, pamoja na rasilimali zake zisizo na kikomo, zimewekwa chini ya amri yetu. Tunapaswa kuchota kutoka kwenye kisima cha wokovu.

Kristo ndiye mwisho wa sheria ili kila aaminiye ahesabiwe haki. Ndani yetu sisi ni wenye dhambi; lakini katika Kristo sisi ni wenye haki.

Baada ya kutufanya kuwa wenye haki kwa njia ya haki ya Kristo, Mungu hututamka kuwa wenye haki, na hututendea k**a wenye haki. Anatutazama k**a watoto Wake wapendwa.

Kristo anafanya kazi dhidi ya nguvu ya dhambi, na pale dhambi ilipozidi, neema inaongezeka zaidi.

"Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo; ambaye kwa yeye tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo tunasimama ndani yake; na kufurahi katika tumaini la utukufu wa Mungu." Warumi 5:1,2

~ AMANI IWE KWENU~

21/04/2022

*SALA YA KUOMBEA MAKOSA YA KILA SIKU*

Baba wa milele, ninakutolea Moyo Mtakatifu wa Yesu, na Upendo wake wote, na Mateso yake yote, na Mastahili yake yote.
Kwanza.
Kulipia dhambi nilizozitenda leo na wakati wa maisha yangu yote. Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, k**a mwanzo na sasa na siku zote na milele, Amina.
Pili.
Kuyatakasa mema niliyoyafanya le na wakati wa maisha yangu yote. Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, k**a mwanzo na sasa na siku zote na milele, Amina.
Tatu.
Kutolea mazuri niliyopaswa kufanya na yale ambayo leo sikuyafanya na wakati wa maisha yangu yote. Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, k**a mwanzo na sasa na siku zote na milele, Amina.

"Mtawa wa Maklara aliyekuwa amekufa, alimtokea mkuu wake mara, aliyekuwa akimuombea, akamwambia "nilienda Mbinguni kwa sababu ya sala hii, kwa kusali kila siku nililipa madeni yangu

21/04/2022

MASOMO YA MISA, APRILI 21, 2022

OKTAVA YA PASAKA, ALHAMISI

SOMO 1
Mdo 3:11-26

Siku zile, kiwete yule aliyeponywa alipokuwa akiwashika Petro na Yohane, watu wote wakawakusanyikia mbio katika tao lile lililoitwa tao la Sulemani, wakishangaa sana. Hata Petro alipoyaona haya akawajibu wale watu, Enyi Waisraeli, mbona mnastaajabia haya, au mbona mnatukazia macho sisi, kana kwamba tumemfanya huyu aende kwa nguvu zetu sisi, au kwa utauwa wetu sisi? Mungu wa Ibrahimu na wa Isaka na wa Yakobo, Mungu wa baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu, ambaye ninyi mlimsaliti na kumkana mbele ya Pilato, alipokuwa ametoa hukumu yake afunguliwe. Bali ninyi mlimkana yule Mtakatifu, yule Mwenye haki, mkataka mpewe mwuaji; mkamwua yule Mkuu wa uzima, ambaye Mungu amemfufua katika wafu; na sisi tu mashahidi wake. Na kwa imani katika jina lake, jina lake limemtia nguvu mtu huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele yenu ninyi nyote. Basi sasa, ndugu, najua ya kuwa mliyatenda haya kwa kutokujua kwenu, k**a na wakuu wenu walivyotenda. Lakini mambo yale aliyohubiri Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake wote, ya kwamba Kristo wake atateswa, ameyatimiza hivyo. Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana; apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa tangu zamani; ambaye ilimpasa kupokewa mbinguni hata zije zamani za kufanywa upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu tokea mwanzo wa ulimwengu. Kwa maana Musa kweli alisema ya kwamba, Bwana Mungu wenu atawainulieni nabii, katika ndugu zenu, k**a mimi; msikieni yeye katika mambo yote atakayonena nanyi. Na itakuwa ya kwamba kila mtu asiyemsikiliza nabii huyo ataangamizwa na kutengwa na watu wake. Naam, na manabii wote tangu Samweli na wale waliokuja baada yake, wote walionena, walihubiri habari za siku hizi. Ninyi mmekuwa watoto wa manabii na wa maagano yale, ambayo Mungu aliagana na baba zenu, akimwambia Ibrahimu, Katika uzao wako kabila zote za ulimwengu zitabarikiwa. Mungu, akiisha kumfufua mtumishi wake Yesu, alimtuma kwenu ninyi kwanza, ili kuwabarikia kwa kumwepusha kila mmoja wenu na maovu yake.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab 8:1, 4-8

(K)Ee, Mungu, Bwana wetu; jinsi lilivyo tukufu jna lako duniani mwote.

Wewe, Mungu, Bwana wetu
Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!
Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni;
Mtu ni kitu gani hata umkumbuke,
Na binadamu hata umwangalie? (K)

Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu;
Umemvika taji ya utukufu na heshima;
Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako;
Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake. (K)

Kondoo, na ng'ombe wote pia;
Naam, na wanyama wa kondeni;
Ndege wa angani, na samaki wa baharini;
Na kila kipitacho njia za baharini. (K)

INJILI
Lk 24:35-48

Wanafunzi waliwapa habari ya mambo yale ya njiani, na jinsi alivyotambulikana nao katika kuumega mkate.
Na walipokuwa katika kusema habari hiyo, yeye mwenyewe alisimama katikati yao, akawaambia, Amani iwe kwenu.
Wakash*tuka, wakaogopa sana, wakidhani ya kwamba wanaona roho. Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu? Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa k**a mnavyoniona mimi kuwa nayo. Na baada ya kusema hayo aliwaonyesha mikono yake na miguu yake. Basi walipokuwa hawajaamini kwa furaha, huku wakistaajabu, aliwaambia, Mna chakula cho chote hapa? Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa. Akakitwaa, akala mbele yao.
Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi. Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko. Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu. Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Want your place of worship to be the top-listed Place Of Worship in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Address


Dar Es Salaam