Catholic_OG

Catholic_OG

Share

04/02/2024

Mtu yeyote anayelipinga Kanisa Katoliki asitumie Biblia, atumie kitu kingine; kwasababu Biblia ni kitabu cha Kanisa katoliki. Historia inadhibitisha hilo kwa sababu Yesu alikuwa haongei na kuandika na wala hakuwa na Katibu na wala hakuacha maagizo ya kuandika Biblia🇻🇦

MAMBO 10 KILA MKRISTO AFAHAMU.
1. Hakukuwa na Biblia kwa miaka 399 BK ya kwanza baada ya Kristo ( Kanisa Katoliki ndilo lililo anza na baadaye ndiyo ikaandikwa Biblia )

2. Kanisa katoliki ndilo lililoamua kuwa na biblia kwa kuchagua vitabu 27 kati ya vitabu zaidi ya 300 vya Injili, nyaraka na kuviita Agano Jipya.

3. Padre Tertullian ndiye alitoa jina la "Agano Jipya" kwa Biblia Takatifu, pia ndiye mwandishi wa Kilatini mzee zaidi.

4. Ni kanisa katoliki ndilo lililoamua ni vitabu vipi viingizwe katika Agano Jipya baada ya kusambaa hati nyingi za uongo.

5. Ni kanisa katoliki ndilo lililotoa Biblia kwa Ulimwengu kwa ajili ya kuwarahisishia waumini wao wakatoliki kujisomea k**a kitabu kimoja chenye vitabu vingi ( Hakukuwa na madhehebu yoyote ya kiprotestant mpaka mwaka 1517 )

6. Mwaka 367 baada ya Kristo, mtakatifu Papa Damasius wa kwanza akiwa na baraza wakati wa upapa wake alichagua hati za maandiko ambazo aliona ni za kweli zilizovuviwa na Roho mtakatifu.

7. Tamko la baraza la Roma chini ya papa Damascus wa kwanza mwaka 382 BK ndiyo lilio halalisha Biblia takatifu.

8. Vitabu rasmi 27 viliongezwa kwenye hati au vitabu 46 vya Agano la Kale na kusababisha mkusanyiko mmoja wa vitabu 73 uitwao Biblia.

9. Mwaka 367 hadi 397 BK mtakatifu Padre Jerome akisaidiwa na Roho Mtakatifu alitafsiri maandiko katika wa miaka 30 na kuiita Biblia Jerusalem. yeye ni padre Mkatoliki, mwanatheolojia na daktari wa kanisa, alizungumza Kigiriki, Kiebrania na Kilatini; Pia alisoma Kiaramu Lugha ya Yesu alivyozungumza.

10. Papa Mtakatifu Siricius ndiye aliyeyaita Maandiko Matakatifu BIBLIA maana yake ni mkusanyo wa vitabu. Na Askofu Mkuu Steven Langton na Kardinali Hugo Desancto Caro wanasifiwa kwa kuunda Sura na mistari au aya katika Biblia yote.

NB
Martin Luther mwanzilishi wa kwanza wa madhehebu kutoka kanisa Katoliki alisema "Tunawashukuru Kanisa Katoliki, Bila Kanisa Katoliki tusingekuwa na Biblia Takatifu" mwaka 1517 ujerumani.

K**a unajivunia kuwa mkatoliki weka "Aminaaaa"

04/01/2024

NJOONI NANYI MTAONA.

*Yoh.1:36-39.*

*Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu!*
Wale wanafunzi .. wakamfuata Yesu. .. Mnatafuta nini?
Akawaambia, *Njooni, nanyi mtaona.* Wakaenda, wakaona akaapo, wakakaa kwake siku ile. Nayo ilikuwa yapata saa kumi.
Umeenda kwake mara ngapi!
Ukitembea wanakusemaje!
Unatembeaje ili wakutambue?
Kwako ni wapi!
Umewapeleka kwa Yesu wangapi!
Umekaa kwake muda wa saa ngapi?

*Anatualika na kutukaribisha, njoni nanyi mtaona.*

Catholic_OG 27/11/2023

Catholic_OG

19/10/2023

Baba Mtakati Francisko amemteua Padre Eusebio Samwel Kyando kuwa Askofu wa Jimbo katoliki la Njombe Tanzania. Alizaliwa tarehe 7 Machi 1964 huko Njombe. Baada ya majiudo yake ya Seminari ndogo ya Mtakatifu Kizito Mafinga, Jimbo la Iringa, aliendelea na falsafa na Taalimungu katika Seminari Kuu ya Mtakatifu Augustine Peramiho.Songea

Na alipewa darala la upadre mnamo tarehe 19 Juni 1996

28/07/2023

*NDOA ZA MSETO NI NINI, NA ZINAFANYIKAJE KATIKA KANISA KATOLIKI?*

Katika Kanisa Katoliki, ndoa kati ya Mkatoliki na asiye Mkatoliki inajulikana k**a "ndoa ya mseto." Ingawa maelezo mahususi yanaweza kutofautiana kidogo kulingana na mahalia pamoja na hali zinazohusika, kuna miongozo ya jumla inayofuatwa na Kanisa katika kesi k**a hizo.

1. RUHUSA KUTOKA KWA ASKOFU MAHALIA
Mkristo Mkatoliki (katika kesi hii, bibi harusi) lazima apate kibali kutoka kwa askofu wa jimbo ili kuolewa na mtu ambaye si Mkatoliki. Ruhusa hii inajulikana k**a "mwongozo kutoka kwa tofauti ya ibada" na inatolewa ikiwa masharti fulani yatatimizwa (Kan. 1125)

2. UCHUNGUZI WA KINA KABLA YA NDOA
Upande wa Mkristo mkatoliki anatakiwa kushiriki katika uchunguzi kabla ya ndoa ili kuhakikisha kwamba yuko huru kuolewa na kwamba wanaelewa wajibu na wajibu wa ndoa ya Kikatoliki.

3. UHURU WA KUTENDA IMANI
Upande wa mtu asiye Mkristo Mkatoliki kisicho cha lazima afahamishwe kwamba Mkristo Mkatoliki yuko huru kutekeleza imani yake na kutimiza wajibu wake wa kidini. Mshirika asiye Mkatoliki anatarajiwa kuheshimu na kuunga mkono imani ya Mkatoliki na, ikiwezekana, kukubali kulea watoto wote katika imani ya Kikatoliki.

4. KUJIANDAA KWA NDOA Wanandoa wanatakiwa kushiriki katika mafundisho ya maandalizi ya ndoa au kuhudhuria ushauri kabla ya ndoa. Hii ni kuwasaidia kuelewa sakramenti ya ndoa, umuhimu wake, na changamoto wanazoweza kukabiliana nazo k**a wanandoa.

5. RUHUSA YA KUOA KATIKA SHEREHE ISIYO YA KIKATOLIKI Katika baadhi ya matukio, askofu anaweza kutoa kibali cha ndoa mseto kufanyika katika sherehe isiyo ya Kikatoliki ikiwa chama kisicho cha Kikatoliki kinafuata mila tofauti ya kidini na ni muhimu. ili wawe na sherehe zao za kidini.

Ni muhimu kutambua kwamba wakati Kanisa Katoliki linaruhusu ndoa mseto na linahimiza Mkristo Mkatoliki kuoa ndani ya imani ya Kikatoliki wakati wowote iwezekanavyo. Hii ni kuhakikisha msingi imara katika imani na maadili ya pamoja, ambayo yanaweza kuchangia ustawi wa wanandoa na watoto wowote wa baadaye.

Inaendelea kwenye comments

Want your business to be the top-listed Clothing Store in Arusha?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Website

Address


Arusha