Msheshe Rashid

Msheshe Rashid

Share

20/03/2026
12/07/2022

Salamu za dhati,

Wanafunzi wa darasa la Nane na gredi ya sita,msijesema hayapo yaliomshinda popo kupapia moyo kichwagoma!
Mia fil mia utabiri wa maudhui
insha na soma la lugha yanaelea viziri tu kwenye visa vya kitabu hiki.Jipatie nakala,usome na ifaidi faida iso kifani.
Wasalaam
Msese wa Kondeni

02/04/2022

MKANDA WA MSIBA.
Msheshe Rashid
Mshale wa saa yangu mkononi, iliashiria muda wa saa tatu na dakika kumi na tatu hivi. Wakati huo,nilikuwa tayari stanini. Nilikuwa hapo asubuhi mbichi ya siku yenyewe. Nilitulia kwenye viti vya steji nikisubiri gari la kuabiri.
Kulingana na kukurukakara za mawio yale, matwana nyingi zilikuwa bado hazijaingia steshenini. Baada ya saa moja,basi nililolitarajia lilifikana kuwasili. Nilibeba kikoba changu na kuingia garini chapuchapu. Nikajichagulia kochi na nikawa abiria wa safari yangu iliyoanza muda mchache la dakika.
Basi nililolichagua,liling’oa nanga . Dereva tuliyemtarjia aliliendesha motokaa. Dereva tuliyemtarjia aliendesha motokaa hiyo kwa ustadi na kasi k**a chui mwindaji. Gari lilitafuna mwendo na kupasua upepo.
Safari ya hatua moja ya gurudumu ikawa masaf ya kitalifa kingi. Mwendo wetu ulizidi kuiva kwenye barabara kuu ya lami hadi pale polisi wa trafiki alipolilegezea spidi kwenye kizuizi cha barabarani. Afisa mmoja wa trafiki aliingia ndani ya basi na kuanza shughuli yake.
Alitupa macho huku na kule . Alishika hap na pale na akachunguza huyu na yule aliyekuwa abiria. Hakuna aliyemshughulikia wala kuma fikira kwa kuwa hiyo ndiyo kazi yake mlinda usalama. Akakagua kwa tathmini zake zote hadi aliponifikia nilipokaa. Nilikuwa nimezubaa zube nikisikia midundo ya ngoma fulani. “ Maisha ni fumbo “ k**a sijakosea.Mwimbaji akiwa Siti Jennifer Mgendi iwapo kumbukumbu zangu hazijatitimia mawazo mengi.
Bahati pengine haikunitunza. Polisi yule aliponifikia,alinikodolea macho. Alinitazama kijeshi kana kwamba nina uhalifu usoni. Hata hivyo sikumrudishia mtazamo wake. Nilitikisa kichwa kwenda na mdundo wa muziki ulionikosha masikioni. Kunifikia mimi ilikuwa mwanzo tu wa matembezi ya ndege mbaya.......
POLISI: (akinitazama kwa makini) Wewe, mbona hauna mkanda?
ABIRIA:Mkanda ninao afisa! (nikionyesha mshipi kiunoni.)
POLISI: (Amekasirika) Sasa unanichezea akili?
ABIRIA: (kwa mshangao) La hasha! Siwezi kabisa! Nimevaa mkanda mkubwa.
POLISI: Yaani hatuelewani. Ebu nionyeshe mkanda wako. Uko wapi?
ABIRIA:Ndio huu hapa askari. Umenikaa vyema kwenye suruali. Mshipi wa ngozi ya mamba.( sijui mbona nilinjibu vile)
POLISI: Kha,Sipendi mzaha! Ebu simama utoke nje! Haraka!
ABIRIA: Ala,nimefanya kosa gani sasam mkuu? Si mshipi ndio huu!Ama....
POLISI: Ama nini? Wewe ongea ukiwa nje kule. Sawa?
ABIRIA: Shida i wapi afande?
POLISI: kijana, kwani hujui mkanda wa usalama? Umenionesha nini? Wewe songa huku. Unaujua mkanda?
ABIRIA: Naufahamu mkubwa.
POLISI: basi! Toka nje una hatia!
ABIRIA: Jamani,basi hili halina mishipi ya usalama. Ningefunga nini?
POLISI: Eti ungefunga nini.! Wewe ni mbuzi ufungiwe kamba!
ABIRIA: Sifanani na mbuzi ama umekuwa chui?
POLISI: wewe ni mjeuri sana sio? Una pembe za ndovu? Ona pale,ile ni kamba ya ajali?
ABIRIA: Hapana. Ni mkanda wa usalama.
POLISI: Vizuri. Umeona kosa lako?
ABIRIA: Sina kosa mzee wangu.
POLISI: Nani mzee hapa? Songa twende nje.
ABIRIA: Subiri basi nishuke taratibu.
POLISI: funga mdomo ndugu yangu. Usijifanye mjuaji.
ABIRIA: lakini,wewe mwenyewe unaliona gari lenyewe. Mikanda haipo kwenye viti vyote. Hatia zangu zi wapi?
POLISI: Hatia ni zake nani? Nani amek**atwa? Ama una chako?
ABIRIA: Afande,tafadhali uwe na huruma. Tena samahani sana,mimi sina chako.m Mwenye hatia ni mwenye gari ama dereva wetu. Ebu muulize kuhusu mikanda.
POLISI: Upuzi. Ngoja ufike kortini ndipo uyaseme usemayo. Mimi sitaki hadithi za Abunuwasi. Nakutia mbaroni.
Aksari aliniingiza kwenye karadinga. Gari la polisi hilo likauma lami hadi kituoni. Huko nilisailiwa kiasi kisha nikaagizwa niingie korokoroni. Nilitulia humo selini nikisubiri hatima yangu ya uamuzi wa tuhuma zangu.
“Askari aliyeshika alidai kuwa nimekaidi kuvaa mkanda wa usalama na kumwonyesha mshipi wangu ulio kuwa ajali kubwa. Pengine nilipitilizwa mawazo. Mungu anifariji,kosa langu lipi?”
Ndivyo nilivyowazia. Mavazi hayo yaliganda pundit tu mlango Wa deli ulifunguliwa.

Want your business to be the top-listed Business in Nairobi?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Telephone

Address


Bahati
Nairobi

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00