Simulizi Za Gilbert

Simulizi Za Gilbert

Share

23/04/2026

Kutoka kwa Mwandishi Halfani Sudy ✍️✍️

Kitabu changu cha saba ni Sanduku Jeusi..

Sanduku Jeusi kinaungana na vitabu vyangu sita nilivyovitoa kwa nyakati tofauti.
1. Penzi Chungu.
2. Farida
3. Kipepeo Mwekundu
4. Kanda ya Siri
5. Msako Hatari
6. Kirusi Kipya

Na sasa ni Sanduku Jeusi.

Sanduku Jeusi kitakufikia popote ulipo nchini Tanzania.

Ni hivi karibuni.

Usipange kukikosa!

15/04/2026

Halfani Sudy
Mwandishi wa riwaya za kiswahili za kipelelezi na kijasusi Tanzania na Afrika ya Mashariki.

"Ahsante Mwenyezi Mungu kwa kipaji hiki..." Halfani Sudy anasema.

Mswaada wake wa riwaya ya Mnara wa Posta umeshika nafasi ya pili katika Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya uandihi bunifu hapo jana Jijini Dar es salaam

Hii ni hatua nyingine kubwa katika maisha yake ya uandishi wa riwaya, baada ya ile ya mwaka 2021 kushika nafasi ya kwanza katika Tuzo za Safal Kiswahili Prize for African Literature kupitia mswaada wake wa riwaya ya Kirusi Kipya (mtoto wa rais)...

Simulizi Za Gilbert inampa hongera na kumtakia kheri kwenye mwendelezo wake wa utunzi na uandishi.

Hebu tuandikie maoni yako hapa, unamkumbuka haswa katika riwaya ipi?

06/09/2025

Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.

Msimu wa Kwanza. Sehemu ya 04

"Unaona pale aliposimama mkuu wa majeshi, Jenerali Evance? hebu nenda mfuate sasa hivi, kuna kijana atakuunganisha nae ili mfuatilie ile helikopta inayoranda angani"

"Sawa Chifu" Elizabeth Neville aliitika na palepale alielekea mahali alipo jenerali Evance.

Alimkuta jenerali Evance akiwa na kijana mmoja aliyevalia magwanda ya kijeshi, mrefu kiasi mwenye mwili wa mazoezi.

"Elizabeth Neville, kutana na Gilbert Mwaitika. Ni kijana wangu ninayemwamini na kumkubali sana. Mtashirikiana k**a alivyokuambia chifu, nadhani mnafahamu ni wapi pa kuanzia, mtafuteni David kwanza mtapata pa kuanzia." Jenerali Evance alisema, Elizabeth Neville na Gilbert Mwaitika walitazamana, wakasalimiana kwa ishara ya kupiga saluti

Upande wa pili alipo Chifu Abdallah Ntenga alionekana akiwasiliana na watu fulani kupitia kisikilizio alichokipachika sikioni. Alikuwa akiwasiliana na maofisa watatu kutoka idara anayoisimamia. Maofisa hao ambao walikuwa karibu sana na Mheshimiwa Rais wakimwekea ulinzi ni Gabriel, Godwin pamoja na Deusderi. Chifu aliwataka Maofisa hawa kumtazama mheshimiwa rais kwa karibu zaidi baada ya kuzuka kwa hali ya taharuki. Yote haya yalifanyika kimya kimya ili kuzuia hofu kwa wananchi na viongozi kwa ujumla ili ziara iweze kutamatika salama. Yote haya yalifanyika kwa weledi mkubwa chini ya usimamizi wa Chifu Abdallah Ntenga, mkurugenzi wa idara ya usalama wa taifa.

Wakati huohuo Mh Eliud Sumbi ambaye ni makamu wa rais alikuwa ametulia kitini akimtazama rais Mark aliyekuwa akizidi kuwahutubia wananchi. Mh Eliud Sumbi mbali na kutulia lakini alikuwa akijilaumu sana baada ya mpango wake kufeli, alipanga katika ziara hii aitumie kumsambaratisha waziri wa Ulinzi Dr Edward Bavu na alishamwandaa mtu maalumu wa kuifanya kazi hii. Alimleta nchini jasusi Ochewa Owechi kutoka nchini Kenya kwa gharama kubwa ili aje kuitenda kazi hii. Mheshimiwa Eliud Sumbi alimfahamu vyema Daniel Mwaseba. Alifahamu ni mtu ambaye hupenda sana kufukunyua mambo. Alipomwona Daniel Mwaseba akizungumza na Chifu na baadae kumwona tena Daniel akitazama upande wa Five Star hoteli aliona mpango wake unaelekea kufeli, alihisi wenda watu hawa wameshanusa harufu ya hatari. Alipomwona mkurugenzi wa idara ya usalama wa taifa akiteta na jenerali Evance aliona mambo yameshaharibika, ikambidi ahairishe mpango wake kwa kumtumia ujumbe Ochewa Owechi ili aweze kuondoka pale haraka. Hakuwa na shaka yoyote juu ya jasusi Ochewa Owechi, aliamini ujumbe aliomtumia kule ghorofani utakuwa umeshatekelezeka.
Lakini hakujua k**a Daniel alishafanya yake, hakujua k**a jasusi huyo kwa sasa yupo katika mikono ya Daniel Mwaseba

Kwa nini Mh Eliud Sumbi anataka kumuua Dr Edwin Bavu? Kuna lipi lililojificha? Ungana nami katika riwaya hii yenye visa vya ajabu, ni mimi mwandishi wako Gilbert Mushi.

*****

Ilimchukua dakika tano tu Dokta Yusha kufika juu ya ghorofa ile, na huko alimkuta Daniel Mwaseba amejiinamia pembeni ya mwili wa Jasusi yule.

"Ooh Mungu wangu! Ni sumu ya aina gani hii inamfanya mtu avimbe mwili mzima kiasi hiki? Sijui k**a atapona huyu labda nijaribu tuu lakini sijawahi kuona sumu k**a hii" alisema Dokta Yusha baada ya kusogea karibu. Alishangazwa na aina ya sumu iliyokuwa katika mwili wa mwanaume yule. Mwili wake ulivimba na kuwa mkubwa k**a unga wa ngano uliotiwa amira na kukandwa kisha kuanikwa juani. Daniel Mwaseba aliinua macho yake kumtazama Dokta Yusha.

"Angeniua huyu, ilinibidi nifanye hivi bwana Yusuph Shaweji" Daniel alisema huku akitaja jina kamili la Dokta Yusha. Dokta Yusha bila kuchelewa alikishusha kibegi chake na kukitua chini, akakifungua na kuvaa gloves

"Mvue nguo ya juu, natakka abaki kifua wazi" Dokta Yusha alimwambia Daniel, Daniel Mwaseba alianza kumvua mwanaume yule koti alilovalia, akamvua na tisheti aliyovalia, tisheti hiyo ilikuwa na picha ya fuvu la binadamu kwa mbele.
Dokta Yusha alitoa visindano vingi vidogovidogo na kuvisokomeza katika kifua cha mwanaume yule, akavisokomeza na visindano vingine katika bega, sehemu ambayo ngumi za Daniel zilitua.

"Nisaidie kupanua kinywa chake," Yusha alisema huku akivuta majimaji kutoka kwenye kichupa kidogo kwenda katika bomba la sindano.
Daniel Mwaseba akatii k**a alivyosema Dokta Yusha, akakipanua kinywa cha mwanaume yule,

"Mmh! Jamaa ana ulimi mweusi k**a wa Ng'ombe, cheki na meno yake," Daniel alisema baada ya kukipanua kinywa cha mwanaume yule.

"Hahaha, hujawahi kumwona mtu mwenye ulimi mweusi? Huwa inatokea, kuna hali fulani ya kibaiolojia inasababisha hivi, kwa wengine ni kutokana na vyakula, na hata maji pia. ila kwa huyu nadhani ni kutokana na mazoezi, anaonyesha amekomaa kimazoezi mno, hali inayonipa matumaini wenda mwili wake unaweza pia kupambana na sumu hii isimshambulie kwa kasi sana" Dokta Yusha akamwelezea Daniel, taratibu akalibinya bomba lile la sindano kuelekea katika kinywa cha mwanaume yule, matone matatu ya mji yakatua katika ulimi wa mwanaume huyo.

"Hii isipomsaidia hatutakuwa na ujanja mwingine tena Daniel, laiti angekuwa mchovu kiafya tungekuwa hatunaye tena huyu hadi sasa, baada ya dakika tano nitavitoa hivyo visindano kisha tutampeleka hospitalini angalau akabadilishiwe na damu maana hii sumu imetapakaa sana mwilini na kuichafua damu yake kwa kiwango kikubwa sana, tutafanya hivyo k**a hiki nachofanya hapa kitaleta dalili njema." alisema Dokta Yusha akimtazama Daniel. Daniel alibaki kumtazama tu bila kutia neno lolote, badala yake alisogelea brufcase ile iliyopo pembeni na kuifungua. Ndani aliona bunduki kubwa ya masafa marefu, miwani ya kumwezesha kuona mbali, pamoja na noti kadhaa za shilingi elfu kumi ya Tanzania. Akahamia katika koti la mwanaume yule, aliona paspoti. Akaikagua kwa makini
"Ni mkenya, jina lake ni Ochewa Owechi, umri wake ni miaka 43." Daniel alisema baada ya kuisoma paspoti ya mwanaume huyu.
"Sasa alikuwa na mpango wa kumpiga nani risasi?" Daniel alikuwa akijiuliza huku akizidi kukagua paspoti ile iliyoambatana na picha. Akaiweka paspoti ile katika mfuko wake. Akazipiga tena hatua hadi katika miguu ya mwanaume yule, akabonyea chini kidogo na kuvua buti zilizovaliwa na mwanaume huyo.

"Mmmh!" akaachia mguno huku mkono wake ukielekea puani kupambana kuidhibiti harufu nzito kutoka kwenye buti zile.

"Ona Daniel, angalia hicho kidude kimedondoka baada ya kumvua buti" alisema Dokta Yusha huku akielekeza mkono wake kilipo kidude hicho. Daniel akainama kidogo kukitazama.

"Kuna watu wanamfwatilia, Ni chipu ya kumwonyesha mahali alipo" Daniel alijibu baada ya kutazama, akaichukua na kutia katika mfuko wake. Dokta Yusha akamshangaa Daniel kwa kitendo cha kukitia mfukoni badala ya kuiharibu na kutupa, lakini Daniel alijua ni kitu gani anafanya

"Najua unashangaa kwanini hivi, ila kusudi langu ni kwamba k**a kuna watu wanamfwatilia endapo wakiona kifaa hiki kimezimika ghafla watahisi huyu mtu ametekwa. Nafanya hivi kuwapoteza maboya k**a watakuwa wanamfwatilia, muda ukifika nitakiharibu" Daniel Mwaseba alimweleza Dokta Yusha.
**********

Kwanini Makamu wa rais ana nia ya kumuua waziri wa ulimzi? Kuna nini nyuma ya pazia? Daniel atafanikiwa kupata chochote kwa mdunguaji aliyetiwa mikononi mwake?
ITAENDELEA KESHO

Want your public figure to be the top-listed Public Figure in Moshi?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Address

Moshi