Simulizi Zetu

Simulizi Zetu

Share

31/12/2025

KEITH - MR ROMANTIC*
*__________________________________________*

*SEHEMU YA KUMI NA MOJA*

Basi wikiendi ikafika salama Nakumbuka ilikuwa siku ya Jumapili. Nilivaa gauni refu jekundu, lina mpasuo pembeni lilinikaa poa ajabu.

Kwa kweli nilikuwa nimependeza sana. Nilipojiangalia kwenye kioo nikagundua mimi ni pisi kali ni kwa vile Jua la bushi lilipausha sana

Baada ya kumaliza kujiandaa, nikatoka. chumbani nikamkuta Keith ananisubiri sebuleni.

Aliponiona mara ya kwanza alishtuka akawa k**a amepigwa na butwaa. lla ghafla tu mood yake ikabadilika akanikunjia sura

"Unaonaje, nimependeza eeeh??" Nilimuuliza kwa nia nzuri tu jamani

"Umependeza but sijui k**a umependeza ivi coz tunaenda kwa Aunt au kwakua unajua Rico atakuwa pale

Nikashangaa "Unamaanisha nimependeza hivi kwa sababu ya Rico?

"Au nimekosea??"

"Kwani Keith Ni kosa kupendeza?? Pia mbona story za Rico tulishamaliza Na mimi sina mda nae kabisa

"Usinielewe vibaya ila Sitaki watu ambao

hawana hatia waumie"

"Watu k**a nani?"

"Watu k**a K**a Maya. Anampenda Rico sana

"Atauumiaje sasa? Nachojua Mimi sifanyi chochote kibaya na Rico. Tumeenda tu kwa sababu wametualika. Na pia ulisema umewa miss Aunt na Uncle unataka kuwaona. Tatizo

liko wapi?"

Hakusema chochote, Alisimama, akachukua funguo za gari akatoka nje hata hakusema Twende. Ilibidi nijiongeze nimfuate nyuma nyuma lasivyo angeondoka aniache

Mnajaua Nikaanza kujiuliza, Kuna nini kinaendelea? Kwa nini ananifanyia hivi?" Ghafla

tu anaanza kuwa k**a mume mwenye Gubu

Au pengine Keith ananipenda? Namna anavyofanya inaonekana kabisa ana wivu. Weeh sikutaka kuamini ila nilijikuta nimefural.

Sio siri hata mimi kuna namna nahisi ninapo kua na Keith. Sijui ni mapenzi au vipi lakini sichoki kumtazama, kumsikiliza mpaka mda mwingine

hadi namwota

Nikajisemea ikitokea k**a Keith atanitongoza

wallah sikatai. Apo najiliwaza ndani ya moyo nikasahau kabisa nina mimba ya mtu mwingine, Ila mimi

Haya Tukafika nyumbani kwa Rico. Tulikaribishwa vizun, lakini baba yake Rico alikuwa safarini. Nyumbani kulikuwa na mama.

yake, Maya na Rico mwenyewe.

Mama Rico aliponiona alishangaa

"Huyu ndiye yule binti wa kijijini?"

Keith akajibu "Si binti kijijini Ana jina lake

Aunt, Anaitwa Lola"

"Amebadilika sana, now kawa mrembo. Ni umaskini tu ndio ulikuwa unamharibu binti wa watu. Angalia alivyo mrembooo...

Maya akaongezea

"Ndiyo si nilikuambia, Lola ni mrembo mno

Walinisifia pale hadi nikaona aibu nikawa

natizama chini tu.

"Sol Mnaendeleaje Kelth? Hujaja kwangu siku nyingi utadhani tuna ugomvi? Mama Rico

alilalamika

"No Aunt si unajua nina jukumu kubwa la Lola! So most of the time nakua busy ofisini, busy

nyumbani but hakuna kilicho aribika! Am sorry

kwa kufanya uni miss sana" alijibu Keith

"Naelewa dr, uzuri leo umekuja No problem So

k**a hamtajali acha niende na hawa warembo jikoni then nyie mka relax huko nje mkisubiri

msosi Mama Rico alituchukua mimi na Maya tukaenda jikoni kwaajili ya kuandaa mapocho pocho

Tukiwa jikoni niligundua mama Rico alikuwa

ananijali sana tofauti na siku ya mwanzo.

Alikuwa mpole mwenyewe nikahisi k**a

ameanza kunipenda

"Usiniogope Lola mimi sing'ati! Najua labda ni kwa sababu ya nilichosema mara ya kwanza

ulipokuja, sometimes mdomo wangu hauna break ila please usiniogope okay??"

Nikajibu "sawa Mama hakuna shida"

"Haya Tupike nini leo?"

"Pilau nyama, kachumban, chips na rosti la kuku alidakia Maya

Mama Rico akacheka "Vyote hivyo?

Maya akasema "Ndiyo, leo ni siku special familia

nzima ipo hapa

"Okay hakuna shida kipenzi tutapika vyote ivyo

Basi Tukaanza heka heka za kupika, ajabu Maya

aliondoka akaenda sebuleni kuchezea simu. Mama Rico hakupenda lakini hakusema.

chochote ili tu asije kukwazana na Maya.

Jikoni Tukabaki mimi, mama Rico na

wafanyakazi wawili waliokua wanatusaidia. Tulikuwa tunacheka na kupiga storil Kale ka

moment kalikua kazuri mno

Mda huo huko Nje upande wa Garden, Keith na

Rico walikuwa kimya kila mmoja na simu yake.

Toka walipandishiane kule restaurant kila mmoja

alikua kamkaushia mwenzake.

Rico alipoona hakuna cha kuongea, akaona ni

heri aje jikoni kuchukua angalau kinywaji. Lakini kabla hajafika jikoni alimuona Maya kakunja nne

sebuleni Akamfuata

"Babe Mmeshamaliza kupika?"

"Me Sijul, Nadhani itakua bado"

"K**a bado hawajamaliza, mbona uko hapa?"

"Unajua sipendi kupika pika nimewaachia wenyewe huko jikoni

Rico akakasirika "Angalau ungeenda kuwasaidia au ukae nao muongee. Hivi unajitenga unadhani

ni sawa?"

"Rico, siwezi hata kukaa kwa amani nyumbani

kwa wakwe wangu? Mama yako hajasema chochote also mimi sio housegirl hapa"

"What??? Maya.. please embua acha drama.

zakol Najua kabisa Mama hajapenda

"K**a hakupenda angeniambia. So please

niache"

Rico hakujibu Akampita akaja mpaka jikoni. Alipofungua mlango, akatuona tukicheka na

kufurahia.

All enjoy kuniona nipo nimejiachia sana na

mama yake. Akatamani ningekuwa mkwe pale

maana nilipatana na mama ake kushinda hata

huyo Maya

Akahairisha kuchukua kinywaji badala yake.

akaenda chumbani kwake na kukaa kitandani.

"Nimefanya nini sasa?? Best wife ni Lola na nilifanya makosa sana kumpuuzia. Najuta hata

kwanini nilipoteza mda wangu kwa Maya...! Daaahinabidi nifanye kitu ili nimpate Maya.

tena lasivyo Keith atanizidi kete"

Rico akawaza kidogo kisha akatoa simu yake, akatafuta namba aliyo isave k**a Patricia,

akaipiga.

Simu ikaita mara mbili then ikapokelewa na Sauti nyororo ya k**e.

"Ah Rico shemeji angu, Inaonekana umeni miss

sana

Rico akasema "Ndiyo, nimekumiss kinomal Unarudi lini?"

"Sijui. Niko bize sana na biashara yangu inaenda vizuri

"Mhhh hongera! Na Vipi kuhusu Keith?"

"Mimi na Keith tuliachana au ulisahau. Nilichagua kazi badala ya kuolewa na yeye

"Lakini bado unampenda

"Ofcourse, Na yeye pia ananipenda. Keith hawezi kumpenda mwanamke mwingine zaidi yangu"

akacheka

"Mambo yamebadilika sasa. Keith anaanza kumpenda mwanamke mwingine"

Patricia akasema kwa mshangao "Nini?

Impossible

"Ukweli ndo huo! Ukichelewa, utamkuta ameoa"

"My God kwanini lakini! Daah so inabidi nirudi haraka lasivyo itakula kwangu! Thanks Rico kwa

taarifal Byeee Patricia akakata simu na kumfanya Rico atabasamu.

Mpango wake ulikuwa kumrudisha ex wa Keith

ili kuharibu kila kitu. Rico alijua Keith alimpenda

Patricia sana.

Walikuwa wanapendana sana na Keith alikua

tayari kumuoa Patricia ila siku moja kabla ya harusi Paticia akapata taarifa kuwa kapata kazi huko Paris ya mitindo.

Kwaiyo harusi ikavunjika Patricia akaenda Paris akimuacha Keith na maumivu. Wallachana

Japo inasemekana bado walikua wanapendana.

Na Patricia alisema akishamaliza kazi zake zote huko Paris atarudi Tanzania kwaajili ya Keith.

Alikua na confidence kuwa hata akimpigia Simu Keith usiku wa manane akiomba warudiane

Keith hawezi kukataa. Yooh nimekwisha mimi

Unajua kitakachofuata? Nakuja

Chapters

Full 1000
Whatsp 0784468229

Want your public figure to be the top-listed Public Figure in Mbeya?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address

Tunduma
Mbeya