AMET AFYA CARE

AMET AFYA CARE

Share

Photos from AMET AFYA CARE's post 15/04/2022

UTANGULIZI – UJUE UGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO

Vidonda vya tumbo ni tatizo linalotokea baada ya kuta za tumbo au utumbo mdogo kuwa na vidonda, hii hutokea ni baada ya kuharibika kwa ukuta wenye ute unaozuia kemikali za kuyeyusha chakula unaoitwa mucus.

Kemikali ambayo ni acidi inayozalishwa mwilini kiasili husaidia kuyeyusha chakula na kuua wadudu tumboni, k**a ukuta wenye ute ukiharibiwa na kushindwa kufanya kazi basi kemikali (acid) itaathiri tumbo au utumbo na kuruhusu bakteria kuendelea kusababisha vidonda vya tumbo.

Vidonda vya tumbo vinatibika kirahisi ila vikicheleweshwa bila kutibiwa huweza kusababisha tatizo kubwa.

Ni tatizo linalotesa sana na kuwanyima raha watu wengi, linahitaji umakini na pia husababisha magonjwa mengine k**a kansa, amoeba (amiba), homa, kupungua uzito.

AINA ZA VIDONDA VYA TUMBO

Kuna aina zipatazo mbili za Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers)

Vidonda vya tumbo kubwa (Gastric ulcers) –

Hivi ni vidonda vya tumbo vinavyotokea ndani kwenye tumbo kubwa

2. Vidonda vya utumbo mdogo (Duodenal ulcers) –

Hivi ni vidonda ambavyo hutokea kwenye utumbo mdogo (hasa juu)

CHANZO CHA VIDONDA VYA TUMBO

Vidonda vya tumbo vina vyanzo tofauti ili vyote ni vile vinavyohusiana na mmeng’enyo, vyanzo hivyo ni;

Bakteria waitwao Helicobacter pylori (H. pylori)
Matumizi ya dawa za kupunguza maumivu k**a asprin, (NSAIDs), (Advil, Aleve, na zingine)
Kuwa na mawazo mengi
Kula vyakula vinavyozalisha acid kwa wingi
Kunywa pombe na vinywaji vikali
Uvutaji wa sigara
Kuto kula mlo kwa mpangilio

Somo kitaendelea

Kwa utahitaji ushauri basi tupige kwa namba

0719658934

Want your practice to be the top-listed Clinic in Dodoma?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address

Dodoma