PR ICON

PR ICON

Share

Photos from PR ICON's post 22/05/2026

PROF NOMBO : SHIVYAWATA YATOA MCHANGO WA MAONI WA MAPITIO YA SHERIA ELIMU, KUKIDHI MAHITAJI YA SASA YA SEKTA YA ELIMU.

Dodoma.

Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia iliyowakilishwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Carolyne Nombo amesema kuwa Tanzania imeendelea kuhimiza wananchi kushiriki zoezi la Ukusanyaji wa maoni ya Mapitio na Maboresho ya Sheria ya Elimu, Sura ya 353 kwa mifumo ya kidigitali na kieletroniki ya tovuti na mitandao ya kijamii ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Leo 22 Mei 2026 - Jijini Dodoma.

Aidha, Katibu Mkuu huyo, Prof. Nombo amesema mchakato huo unalenga kuhakikisha sheria mpya ya elimu inakidhi mahitaji ya sasa ya sekta ya elimu kuwa nyumbufu na shirikishi ikitoa nafasi kwa wananchi kutoa maoni hadi mwezi Juni kabla ya hatua za mwisho za kuwasilisha mapendekezo katika ngazi za maamuzi iinayojumisha Kamati ya Elimu, Utamaduni na Michezo kwa ngazi ya Bunge.

Mkutano huo uliodumu kwa siku mbili (2) umeshirikisha wadau muhimmu kutoka Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) wamepongeza ushirikishwaji huo na kusisitiza umuhimu wa elimu jumuishi, matumizi rasmi ya lugha ya alama katika ngazi zote za elimu, na kuhakikisha hakuna mwanafunzi mwenye ulemavu anayeachwa nyuma.

Photos from PR ICON's post 21/05/2026

MHE. WANU: ASISITIZA MATUMIZI YA MIFUMO KIDIGITALI, KUSANYA MAONI YA KUBORESHA SHERIA YA ELIMU - NCHINI.

Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir (mb) amesema Serikali inaendelea na Mapitio ya Sheria ya Elimu Sura ya 353 ikishirikisha wadau mbalimbali wa elimu kwa lengo la kuhakikisha sheria hiyo inakidhi na. kuendana na mahitaji ya sasa ya kisekta, Mabadiliko ya Sera, maboresho ya Mitaala na Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia.Aidha, Mhe.Wanu akizungumza Leo 21 Mei 2026 - Jijini Dodoma kupitia Kikao cha Wadau wa Kujadili Taarifa ya Awali ya Mapitio hayo, amesisitiza umuhimu wa wadau kuendelea kutoa maoni yao kwa uhuru na uwazi, ikiwemo kupitia tovuti ya Wizara.

Photos from PR ICON's post 21/05/2026

WIZARA YA UJENZI : SERIKALI KUJENGA ZAIDI YA KILOMETA 1,495 KWA KIWANGO CHA BARABARA YA LAMI HADI KUFIKIA 2026/31.

Dodoma.

Waziri wa Ujenzi, Mhe. Abdallah Ulega (mb) amesema Serikali ya Awamu ya Sita (6) inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inatarajia kujenga Kilometa 1,494.45 kiwango cha Lami na Madaraja makubwa 18 kwa miaka mitano (5) wakati akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha wa 2026/2027, hatua itakayoimarisha miundombinu ya Sekta ya Usafirishaji kuwa fungamanishi na kuchochea ukuaji wa Uchumi.

Mhe. Ulega amesema, Mtandao wa Barabara za Kitaifa (Road tarmac) unaoratibiwa na Wakala wa Barabara TANROADS umefikia Kilometa 37,734.41 ambapo Kilometa 12,225.26 zimeshajengwa kwa kiwango cha lami. Aidha, Amefafanua wakati Tanzania inapata uhuru mwaka 1961 nchi nzima ilikuwa na Kilometa 1,360 pekee kwa Barabara za kiwango cha lami, huku Serikali ya Awamu ya Kwanza (1) mpaka Awamu ya Tano (5) zikijenga jumla ya Kilometa 9,369.81. Hali inayoonesha Kasi kubwa ya Maendeleo ya Miundombinu katika Ukanda wa Afrika Mashariki ikiwa ni Mafanikio yanayoendelea kutekelezwa na kushuhudiwa na Serikali ya Awamu ya Sita (6) nchini.

Aidha , amebainisha kuwa Katika Utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka 2025/2026 Wizara ya Ujenzi ilipanga kujenga na kukarabati Kilometa 450 za Barabara kuu na Mikoa za Kilometa 820 kwa kiwango cha lami na Changarawe. Hadi kufikia Aprili 2026, Serikali ilikuwa imeshakamilisha ujenzi na ukarabati wa Barabara za Kiwango cha Lami za Kilometa 94.36 za changarawe. Pia, Serikali imeeleza kuwa Utekelezaji huo unafungamana na ongezeko la Juhudi na Ubora wa miundombinu ya Usafiri ili kukidhi mahitaji ya wananchi kwa kurahisisha na kuharakisha ukuaji wa shughuli za kiuchumi.

Kwa upande wa Ujenzi wa Miundombinu ya Madaraja , Mhe. Ulega amebainisha kuwa Serikali imekwisha kamilisha jumla ya ujenzi wa Madaraja Tisa (9) ikiwemo Mitomoni (Ruvuma), Mirimba (Katavi) , Nzali (Dodoma) , Kaleba (Kagera) na Itembe (Simiyu) na ujenzi wa madaraja 11 unaendelea huku Serikali ikiandaa miradi mipya ya madaraja 13 ikiambatana na Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa miradi mbalimbali. Aidha, Serikali imesisitiza miradi hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa uimarishaji miundombinu ya Kisasa na kuongeza fursa za ukuaji wa uchumi wa ndani ya nchi kwa kurahisisha shuguli za kijamii na kiuchumi nchini.

21/05/2026

KITUO CHA TAFITI ZA FIKRA ZA XI JINPING CHA UJAMAA CHAZINDULIWA, KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUELIMU NA MAENDELEO YA CCM NA CPC.

Dar es salaam.

Viongozi kutoka Vyama Sita (6) Rafiki Kusini mwa Afrika wameshiriki Uzinduzi wa Kituo cha Tafiti kuhusu Fikra za Xi Jinping juu ya Ujamaa wenye Maono ya Kichina katika Zama Mpya, hatua inayolenga kuimarisha ushirikiano wa kielimu na maendeleo kati ya CCM na CPC.

Photos from PR ICON's post 20/05/2026

MATUKIO

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ,(mb), amekutana na kufanya mazungumzo na mchezaji wa zamani wa Timu ya Taifa ya Uingereza na Klabu ya Manchester United, Ndg.Rio Ferdinand katika kikao kilichohudhuriwa na viongozi kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Mei 20, 2026 - Jijini Dodoma.

Want your business to be the top-listed Media Company in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address

Kimara
Dar Es Salaam
1061