Mshauriwaafya

Mshauriwaafya

Share

08/02/2022

Njoo Tukusaidie
+255746525852

01/01/2022

MAUMIVU MAKALI YA NYAYO NA KISIGINO (PLANTAR FASCIITIS/POLICEMAN HEELS); UGONJWA UNAOWALIZA WATU WENGI WAKATI WA ASUBUHI.
Na Williams 0746525852.

Maumivu makali ya nyayo na kisigino(Plantar fasciitis /policeman heels) ni tatizo linalotokana na kuwepo kwa maambukizi yanayojumuisha kuvimba kwa bendi nene ya tishu ambayo hupatikana katika nyayo zetu miguuni,ambayo ndiyo inaunganisha mfupa wa kisigino na vidole vya miguu yetu (Plantar fascias).

Maambukizi katika bendi nene ya tishu zinazopatikana miguuni ambayo inaunganisha mfupa wa kisigino na vidole vya miguu yetu husababisha maumivu makali ya nyayo na kisigino(Plantar fasciitis).

maumivu makali ambayo mara nyingi hutokea asubuhi pale muhusika anapoamka na anapoweka miguu yake chini na kuanza kupiga hatua zake za kwanza asubuhi,maumivu huwa makali sana ambayo hupungua kadri anavyopiga hatua lakini pia hali ya maumivu huweza kurudi baada ya muda mrefu wa kusimama au unaposimama baada ya kukaa.

maumivu makali ya nyayo na kisigino (Plantar fasciitis) huweza kuwapata watu wa rika zote ingawa hutokea zaidi kwa watu wanaofanya mazoezi ya kukimbia sana kadhalika watu ambao ni wenye uzito mkubwa sana na wale ambao huvaa viatu visivyo na visigino na wale wanaovaa viatu vyenye visigino virefu mara kwa mara.

CHANZO CHA MAUMIVU MAKALI YA NYAYO NA KISIGINO

Inakadiriwa kuwa wanawake na wanaume walio katika umri wa miaka 40_70 wapo katika hatari kubwa ya kupata tatizo hili la maumivu makali ya nyayo na kisigino (plantar fasciitis), kadhalika wanawake wameonekana ndio wahanga wa kubwa wa tatizo hili la maumivu makali ya nyayo na kisigino ( plantar fasciitis) kuliko wanaume pia wanawake wajawazito nao wamekua wakisumbuliwa na tatizo hili vipindi vya mwisho vya ujauzito.

Mpendwa msomaji ili uweze kuelewa chanzo cha tatizo hili napenda kukujuza kua katika miguu yetu kuna tishu nyembamba ndefu inayopatikana katika maunganio ya nyayo na kisigino ambayo iko moja kwa moja chini ya miguu yetu,tishu hii inasaidia upinde wa mguu wako na kutusaidia hasa wakati tunapotembea au kusimama.

Lakini Iwapo kutatokea mvutano na msukumo mkubwa juu ya mishipa, mvutano au msukumo huo mkubwa huharibu tishu hiyo na kupelekea kupatikana maambu

Want your business to be the top-listed Grocery Store in Arusha?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Telephone

Address

Sekei
Arusha

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00